TEVEZ APATA MAPOKEZI MAKUBWA ITALIA TAZAMA PICHA.


 


MSHAMBULIAJI Carlos Tevez amewasili Italia na kupata mapokezi makubwa kuelekea uhamisho wake wa Pauni Milioni 10 Juventus kutoka Manchester City.
Mpachika mabao huyo wa Kiargentina alitua katika Uwanja wa Ndege wa Malpensa mjini Milan na kupokewa na umati wa mashabiki ambao mara zote hupenda kuwalaki nyota wao wapya.Tevez, mwenye umri wa miaka 29, anataraji kusaini mkataba wa miaka mitatu jijini Turin baada ya vipimo vya leo huku makubaliano yakiwa yamefikiwa. 
*ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU*

No comments:

Post a Comment